Wednesday, October 12, 2005

Makosa na usahaulifu.

Barua niliyomwandikia ndugu yangu nkya, sijui kam inaukweli ndani yake au inaweza kutumika kuombea PHd kwenye fani ya siasa.
Ndugu Hilo ndilo kosa la ANC naona liko kama kosa la Nyerere, yeye hakuamini kama ujamaa unaweza kuanguka, ilikuwa ni dhambi kama kufikiria kuwa papa. Alijenga mashirika ya umma bila kuwapa umiliki wananchi hivyo ujamaa ulipoanguka na hayo mashirika yalishindwa kuendeshwa na wananchi, sasa wakipewa wazungu kuyaendesha tunapiga kelele bila kutafuta chanzo, angalia wachina naona mao alijuwa hiki kitu akaandaa watu wake ili kuwa tayari kumiliki uchumi iwapo ukomunisti ungeanguka ndiyo maana wachina hawanashida na mwekezaji toka ulaya.Kila mchina ana uwezo wa kutengeneza kitu ambacho sisi tunatumia dola nyingi kuviagiza. Sijui fani yako, lakini naona kama sio technolojia ya chuma uchumi wa ulaya usingekuwa hapo ilipo sasa, wameweza kutengeneza vyombo vya usafirishaji, mitambo na pia vifaa vya kilimo vilivyowapatia maendeleo ya haraka. Sijui kama wangengoja wa-kushi wawatengenezee hivyo vifaa wangekuwa wapi sasa?. Sina takwimu sahihi lakini naona kama technolojia ya chuma hapa Tanzania haithaminiwi ndio maana tunaingia karne ya 21 bado tunatumia jembe la mkono!. Marekani iliendelea kwa kuwafanya waafrika watumwa wao kwenye mashamba na migodi, hilo sisi hatuliwezi, lakini tunao ng'ombe wengi wenye nguvu kama nyati kwa nini tusiwatumie kukuza kilimo? Ukinichagua mimi nitaleta maendeleo bila wananchi kujifunga mkanda, ghafla mahitaji yatajaa madukani, na pesa mifukoni hawaongelei, ukweli ni havitakuwa vya waliowapigia kura! Angalia ikapa hapo, huna haja ya kuwasha gari kwenda kazini, unauhakika wa kupanda treni au kama ni mwoga 'Golden arrow' ipo. Nini maana yake 1. Unakuwa umetunza mazingira kwa kutotengeneza moshi mchafu kuliko ukoma. 2. Umepunguza mafuta ambayo serikali hutumia mamillioni ya pesa za kigeni kuyaagiza baada ya kuhudumia wakulima na sekta nyingine zenye umuhimu. 3. Badala ya kuendesha gari ukiwa peke yako na kuleta msongamano mjini, utaupunguza kwa kutumiausafiri wa jumuiya- ambao ni nafuu zaidi kwa gharama.
Hayo ndiyo maoni yangu. Mjadala uko wazi kuchangia.

Wednesday, October 05, 2005

Samahani

Nimejaribu kualika watu pasipo na viti, samahani nilisahau, nafasi za watu kukaa. Walikuja wengi sana wakakuta hakuna nafasi ya kukaa hata mtu mmoja, sijui kama waliondoka kimyakimya kama mchungaji anaposisitiza watu wachangie sadaka nyingi zaidi au walitukana kama siku yanga ilipofungwa na simba.
Unajua kila kitu kina aina yake, kama vile wengine huandaa tafrija ndipo waalike watu kusheherekea kwa kunywa na kula lakini wengi hualika watu kuja kusaidia kuandaa tafrija hata kama haiwahusu au haina ulazima kwao wanatakiwa "kuchangia" ili ifanikiwe. Samahani hivi mimi ninaonekana niko kwenye kundi lipi?
Habari huandikwa na mwandishi wa habari lakini mimi sio mwandishi wa habari wa kuandikia watu, nataka watu waniandikie mimi nizisome habari zao, mko tayari kuniandikia bila malipo? Je watu hupenda kusoma kila habari iliyopo, sijui kama ukimwanbia Rasta afrika siyo kwao atakusadiki, labda ukitumia njia nyingine ambayo sijawahi kuisikia .
Habari zipo nyingine ni nzuri na nyingine ni mbovu nani anajua habari iliyo nzuri kila wakati, kama ni hivyo waandishi wasingekuwa wanazeeka na kujiuzulu kila siku au kufukuzwa kazi kwa ufanisi mbovu.Sio kama sikubaliani na uwapo wao, ila nahitaji kuwa na busara zaidi ya ile ipatikanayo toka kwa mmoja mmoja.
Kaa tuongee nilikuta nyumba ya wageni moja pale livingstone nchini zambia inaitwa tulye tonje nikaambiwa maana yake ni kaa tuongee, sijui kama itakuwa na uhusiano na hii kaa tuongee, hapa panaendeleza na hatufanyi mambo ambayo yatamdhuru mtu, sikumbuki kilichokuwa kinafanyika tulye tonje, maana nilifika usiku na mchovu wa safari hivyo nilifurahia kupata kitanda kama nimefika safari yangu.
Karibuni tukae tuongee, kila mmoja ashiriki katika maongezi haya tupate kilicho kweli hata kama kitawauma wengi na wachache wengine wajue kwamba wamekalia misumari na wasiponyanyuka haraka itawachoma washindwe kukaa kesho kama kesho huwa inafika.