Wednesday, November 23, 2005

Tunapinga na kupinga...

unajiita sauti ya wanyonge,
lakini muda pekee unapotoa sauti yako
ni pale unapopinga walichosema wenzio....
Bahati dube, wimbo: mchezo wangu (my game).

Nimekumbuka wimbo wangu kipenzi toka kwa gwiji la reggae dube, sijui kama wimbo huu uliwahi kupata tuzo, labda ni muendelezo wa hadithi za muziki wa kitumwa wa kisasa zilizoanziswa na msangi, ndesanjo jeff na nkya kudakia.
Wanablogu tunataka kuingia kwenye hali hii, tunajifanya kwamba ni sauti za wanyonge lakini kumbe tunachofanya ni kupinga wanachofanya wenzetu, sijui tuna wivu sana kwa kukosa maendeleleo kama wao ama ni kutaka kuwa juu ya watu wote!
Wenzetu wa kizazi kipya, kisichojua tofauti ya uhuru na utumwa, Utamaduni na hadithi, Chao na cha wenzao, mwanzo na mwisho.... na kuuita muziki wa kizazi kipya, kama tulivyo tumedakia na kuupigia kelele wakati hata siku moja hatujawahi kuwaonyesha mathalani kuwafundisha muziki wetu uko vipi, Sembuse kuwapa nafasi ya kutatua matatizo yao kupitia muziki WETU, tunatarajia vijana kuupenda muziki wetu na kuacha mingine inayowafikia kwa urahisi kuliko yetu.
Tuliangalia Mashirika ya umma yakiteketea, bila kufanya juhudi za kuyaokoa,siyo kulia tu ila kwa kujitolea hata damu kuyatetea kama mashahidi wa uganda walivyomtetea yesu kwa kabaka, tuliona ni sawa tu kwanza hayatupunguzii kitu na wala hayatuhusu!, ukweli ukaonekana kwamba tunahitaji yawepo kwani huduma zake zilihitajika sana, serikali ikaona njia pekee ni kuyabinafsisha lakini wakaanza sasa yanafanya uzalishaji kwa ufanisi wanablogu tunalia nchi imeuzwa! labda kati ya aliyeiua na anayeiuza ili ifufuliwe, wapili ni mbaya zaidi.
Serikali kivuli nayo iko kama wanablogu, wanaingia bungeni bila mipango, halafu ni mabingwa wa kukataa, ili wawape lawama serikali ikishindwa kwenye mipango yake. tunakuwa mabingwa wa kuchambua mipango ya wengine wakati hatuna yetu, Ila tunamawazo yanayopinga maamuzi ya wengine ingawa nayo pia tunayapanga tukiwa usingizini bila kuwashirikisha wanaolengwa na mipango hiyo. Sijui kama tukifanya sensa leo ya mambo yanayoandikwa kwenye blogu, mangapi yatakuwa sio mawazo binafsi ya mwanablogu aliyeyaandika? tukiendeleza sensa hii na kuangalia ukubalikaji wa hoja za blogu, sijui kama kutakuwa na hoja zao ila tu zetu hazipewi nafasi kwa sababu hatuna dola ya kuzisimamia. katika pitapita yangu kwenye vibaraza vingi nimeyaona haya, kila mahali wanamambo wanayoyapenda, ila hakuna kibaraza kinacholengana ma mawazo ya serikali!
Mwanamapinduzi Walter Rodney alianza kuishinda hali hii, kwenye mafundisho yake aliyaita "grounding with my brothers" aliwakusanya vijana na wanamapinduzi kisha kujadiliana nao, hii iliamsha ari yao ya mapinduzi na kumfanya rodney awe chakula cha risasi.
tuangalie sisi tufanye nini.