Tuesday, May 23, 2006

Mkaribisheni mgeni.

Kamala Godwin amependezewa na blogu zinavyofanya kazi, ameamua kujiunga kwenye mtandao huu, yeye anapatikana hapa mtembeleeni.
Hawa wameumbwaje?

Burning Spear aliuliza hivi, ….Unakumbuka siku za utumwa? Babu zetu walivyochukuliwa kama vifaa vya kufanyia kazi. Wengine wengi mpaka leo wanahoji hivi utumwa ulikuwa halali? Maswali huwa hayaishii hapo tuu, mengine mengi hufuatia kama vile ukiwa Afrika na makazi ya waafrika kote duniani utasikia maneno haya …..Unajua hawa watu wa ulaya wanatunyonya sana! Ukiwa kwenye maeneo ya wazungu ukikutana na waafrika wengi wao watakwambia Unasikia bwana hapa tatizo kubwa ni kubaguliwa, tunachukuliwa sisi (waafrika) kama watu wa daraja la chini sana … Ukikuta maraisi wa Afrika kwenye mkutano wataongelea tofauti katika mgao wa biashara baina ya nchi za Afrika na za magharibi( Ulaya na Marekani) hawa hujadili njia madhubuti ya kuleta usawa na kuzinufaisha nchi za kiafrika katika biashara ya dunia.
Dunia nzima na sasa hata watoto wao wazungu sasa wameanza kuwasema baba, mama, babu na bibi zao kwa wanachowafanyia waafrika na wa-Asia kiasi cha kujitolea maisha yao kupambana na Dola zao. Lakini wengi wao hawatajibu au kufanya lolote kuhusu jambo hilo na wala hawatachukia maneno yako wala kuyafurahia.
Ukimsikiliza Tony Blair , Joji Kichaka na wengine wa aina hiyo watakubali machono mwako kwamba waafrika wanadhulumiwa na kuna haja ya kufanya mabadiliko ili kubadili mfumo uliopo sasa na kuahidi kutoa kipaumbale kwa jambo hilo.
Wataunda kamati za kushughulikia jambo hilo lakini matokeo yake yatakuwa labda hawataongelea tena matokeo ya kamati hiyo au ufumbuzi utakaotolewa utaleta matatizo na manung’uniko mengi zaidi!
Cha kushangaza ni uvumilivu wa wazungu kuhusu kauli zinazowakosoa na manung’uniko wanayopata kutokana na matendo wanayowafanyia watu wa asili nyingine tofauti na zao. Nashindwa kuelewa uumbwaji wao ulikuwa wa aina gani kwani sisi waafrika tukisemwa kidogo huwa tunajirekebisha na kufuata ushauri tuliopewa na “wenzetu”.

AU, NEPAD NA Viongozi

Nimesoma mawazo haya kwenye NewAfrikan na kushangaa kweli kuhusu ukweli wa saga la Charles Taylor. Sijui huku kugeukana kutaisha lini!. Bonyeza hapa usome na mimi.

Thursday, May 18, 2006

Unawasikiliza hawa?






Ndesanjo ametuwekea kiunganishi kwenda kwa baadhi ya watu hawa lakini sidhani kama huwa tunajaribu kuwapitia. Hawa ni washairi wa ki-reggae wanachanganya usomaji wa mashairi na midundo ya reggae katika hali fulani ambayo inapendezesha sana mashairi yao.

Kushoto kabisa anaitwa Michael Smith yeye habari zake nyingi hazijulikani sana lakini niliwahi kupata kazi yake moja kwenye shairi la 'me cyant believe it' na lingine ambalo sikumbuki jina lake. Inasemekana kutokana na msimamo wake dhidi ya chama kilichokuwa kinatawala na ukali wa maneno yake wafuasi wa chama tawala kule Jamaika walimvamia akiwa sokoni na kumponda mawe mpaka mauti yalupompata.

Hizo mbili za katikati ni Mutabaruka maarufu kwa mashairi ya ukombozi, Yeye habari zake zipo kwenye kiunganishi katika jina lake. Nakumbuka alipohojiwa kwenye muhutasari wa maisha ya Peter Tosh alisema kwamba... unapodai haki yako huhitaji kujadiliana na mdaiwa wako maana unakuwa unaipoteza haki yako..... na katika mahojiano mengine alisema ..... Afrika inasubiri waumbaji wake.... Jaribu kumfuatilia.

Picaha ya mwisho wako wawili, kushoto ni Benjamin Zephaniah, maarufu kwa mashairi na mweusi ambaye alikataa tuzo ya OBE aliyopewa na Malkia lizabeth, rudia siku Beckham alipopewa tuzo hiyo, kwa madai malkia hawajali waafrika ili anajikomba kwake. Kulia ni Linton Kwesi Johnson, aliyeshangilia upinzani dhidi ya ubaguzi wa weusi uingereza, katika shairi hilo alisikika akisema, .... kidonge cha ukandamizwaji kilitapikwa na polisi wawili walikufa..... kama ishara ya ushindi dhidi ya ubaguzi.

Wote wanne ni wazaliwa wa Jamaika .Mutabaruka yeye anaishi Jamaika, Kwesi na Benjamin Zephaniah wanaishi uingereza.

Tuesday, May 16, 2006

Miaka 25 ya kifo cha Bob Marley...

Wiki iliyopita kulikuwa na sherehe na matamasha ya kumkumbuka gwiji la reggae Bob Marley, kama anavyojulikana na wengi,
mwingine alifanya kumbukumbu hiyo kwa njia nyingine, Huyu sio mwingine bali ni rafiki wa karibu sana wa Bob Marley na mpiga gitaa wake maarufu Aston Barret au "Family man". Kumbukumbu yake ilikuwa ni kukumbuka jinsi alivyosaidiana na Bob na wengine wanavyofaidika siku hizi na yeye na ndungu wa marehemu mdogo wake walivyoachwa masikini bila kukumbukwa, madai yaliyomfanya afungue kesi mahakamani na nakala ya hukumu yake
hii hapa .

Thursday, May 04, 2006

Moto moto moto kila mahali ....

Nimejaribukuweka tena viunganishi nilivyokuwa nimekosea kama mlivyonishauri na sasa viko fiti kwa kufanyiwa tizi. Angalia nakala iliyopita ya blogu kila mahali ujionee ilivyo.
Picha pia zimeanza kuonekana unaweza kuona nyingi zaidi kwenye flickr Lakini hii isimtishe Michuzi kwamba staili yake imeingiliwa na kupikuliwa, bali imehamasisha blogu nyingine zaidi. sijui Mpoki Bukuku alihamasishwa kwa muda tuu!( just a passing glance) Motowaka hata "share a moment" na michuzi ataishi pale.

Ingawa sasa nimebadilika kidogo, Hii ilikuwa Mwaka 2003 Nilipokuwa picha ya kwanza Capetown na ya pili kwenye basi Livingstone, Zambia. Bado najilaumu kwa kutopiga picha nyingi na nzuri kuliko hizi.