Tuesday, January 10, 2006

Salaam ndugu...., habari za nyumbani? watoto?

Fikiria maisha yatakuwaje iwapo pale utokako nyumbani asubuhi kila uingiapo salamu zitafuata mlolongo huu.

Uingiapo kwenye Daladala unaanza kumsalimia mpiga debe ndugu habari za kuamka, nyumbani hawajambo, mama? watoto? halafu unahamia kwa konda, Habari gani? Vipi kazi leo? imeanza vizuri? mbona unaonyesho uchovu asubuhi hii yote? hukulala nini?. Naye konda anaanza kupita kwa kila mtu habari kaka/dada, Leo umechelewa kutoka? au mabasi ya shida leo? poleni sana, naomba nauli.

Mwendo unakuwa huu huu kwa kila unayekutana nae siku hiyo muuza chai, muuza machungwa,walinzi, makarani wa benki, watu wanaofanya promosheni maofisini na ndugu zao machinga, bila kusahau unaingia kwenye blogu zote unaweka salamu za asubuhi kwa kila moja.

Fikiria tena utatumia muda kiasi gani kutoa hizo salamu zote! utakuwa katika hali gani? utaweza kuendelea na kazi siku hiyo? Kazi ngapi zitasimama? foleni itakuwa kubwa kiasi gani?.

hivyo ndiya watu wanavyotaka iwe siku yao na wewe pia uwaige .