Friday, February 24, 2006

Bado nipo..

Sio kama nimeondoka kimyakimya bado nipo ila mambo yaliingiliana kidogo ndiyo maana niko kimya. Wordpress imekuja kwa kishindo kama ilivyokuja Blogspot inatamanisha kuhamia kwenye hayo makazi mapya, bado ninafikiria kama yatakuwa mapya siku zote au ndiyo kilekile, kipya kinyemi na kuwa wa kileo hata kama hujafika leo!
Ndio ninapata matatizo kidogo kutumia blogspot, mpaka leo sijaweka picha yangu hapa,labda nimezoea "cut and Paste" iliyorahisi bila kuzungukia njia nyingine, lakini hapa tunapendana zaidi kupaacha sio rahisini kama kukubali kufa na kuwaacha uwapendao dunuani.
Mijadala inazidi kupanuka, kila kitu kinawekwa wazi hapa. Kuna kusanyiko la waandishi wa habari, wasomaji wa habari wanaopenda kugawia wenzao habari walizoziona kwenye sehemu mbalimbali, watu wa soga, watuma picha na wa udaku pia. Wanablogu wa kiswahili tumeungana kwa kiasi kikubwa, sote tunashirikiana na kujuana kwa majina ingawa hatujuani kwa sura, siwezi kusema kwamba hakuna wanablogu wa kiswahili walionje ya mtandao huu.
Blogu nyingi zimevuma hapa wakati kama hii yangu inatokea kwa nadra na bila viunganishi motomoto, ukitaka viunganishi motomoto unaweza kupitia makene, ndesanjo , Nambidza na kuzunguka kwenye blogu zote za kiswahili zilizo kwenye mtandao huu.
Ushirikiano na kutembeleana kati yetu tuuendeleze, tusiwaache wenzetu waliohapa maana wametueleza walipohamia hivyo bado tupo nao, tuwatembeleeni ili tuendelee kufaidika na mawazo na ufahamu wao.