Wednesday, March 29, 2006

Vibaraza vinaendelea.....

Vibaraza bado vinaendelea, kuna kipya cha Simba na Yanga lakini mwenyewe hasemi kama ni Simba au Yanga ,mimi naona kakaa kama Yanga vile,
Mtembelee hapa. Umuulize yeye ni simba au yanga, asipojibu shauri yake.
Mwandani sasa ameweka picha yake lakini sio mojakwamoja kama humjui huwezi kujua ni nani yule, lakini binti Simba anatuambia
huyu ni mwandani. Hilo afro bado lipo kama siku tulipoachana Tambaza Boys sekondari.
Yule mnakala maarufu wa mwananchi, Yahya cherehani na yeye pia ameingia kwenye blog,Naona sasa blog zinateka watu wote waume kwa wake wenye habari motomoto. Yeye
anashona kuliko cherehani ya mchina bila kutia umbeya na uwongo wa wanasiasa.
Ndesanjo naye kwenye nyumba yake mpya mambo bado ni moto sana.
Angalia kesho vibaraza vitakuwa vipi.