Saturday, August 19, 2006

Maamuzi na Maazimio

Unafanya maamuzi na kuyatimiza!
Unaamua nitakuwa nakula mara moja kwa siku ili niushinde ugonjwa wa "obesity" unafanya hivyo mpoka unazoea na 'obesity' haiwi tena tatizo la kusumbua akili yako.
Unaamua kuwa kibaraka, unakuwa na kutajirika kwa gharama ya waliokuwa wazalendo wenzako.
Unaamua kuwa wa dini hii, na unakuwa.
Unaamua kutovaa viatu kwa sababu zako na unaacha kuvaa viatu kama alivyofanya Mutabaruka.
Hata kama huwezi kuwaeleza wengine wakubaliane na maamuzi yako lakini hayo ndiyo maamuzi yako mwenyewe na unaamini yanamanufaa kwako.
Tatizo kubwa ni pale unapofanya maamuzi yako na kuyatekeleza kwa gharama za wenzako na bila ridhaa yao hata kama watayakubali kwa kuburuzwa ndipo yanakuwa sio maamuzi mazuri.
Wiki chache zilizopita Dunia ilikuwa kwenye kilio kikubwa kutokana na vita ya Hamas Na Israeli, ingawa sasa mapigano kwa kiwango kikubwa sana tunasema yamesimamiswa lakini inabidi tuliangalie suala hilo sasa, nini kilileta mapigano hayo? Ardhi ya waarabu, uchokozi wa Hamas, au ubabe wa waIsraeli? Hakukuwa na njia nyingine ya kufuata kutatua matatizo hayo zaidi ya kusababisha mauaji ya maelfu ya watu? majibu ni mengi kuliko maswali.
Ukiamua kujenga nyumba yako mabondeni mimi hainihusu mradi tu usizibe ule mto ufanye kipindi cha masika maji yafurike mpaka nyumbani kwangu.
Hawajama walioamua kuwa 'mateja' haituhusu kama hawatatuingilia, tunapiga kelele sababu hawana njia nyingine ya kupata pesa kwa ajili ya hiyo starehe yao zaidi ya kuvunja nyumba zetu, kutuchomolea mifukoni kutukaba na hata kutudhuru hadi kifo, kama watakuwa na njia nyingine za kutimiza strehe zao nadhani tusingejali sana ilimradi hawakai kwenye mapito yetu kama takataka(kwa uchafu) zinazosubiri kupelekwa dampo na kutubughudhi.
Ukiamua kuwa masikini asiye na malengo hakuna atakayekuingilia, ila wanasiasa fulani watatumia hali yako kujipatia umaarufu kama hutakuwa thabiti kwenye maamuzi yako.
Mtoto akiamua asipende kusoma kwa sheria za sasa mwalimu hatahangaika kumfuatafuata, jua hakielimu wanapigia debe walimu wasiruhusiwe kuchapa viboko bila kutoa njia mbadala kwa mazingira ya Tanzania, akiogopa sheria na kujua mwisho wa mwezi mshahara ni uleule wa kutumia wiki mbili aanze tena kukopakopa.
Ukiamua kuwa hivi kuwa mradi huwaingizi wengine kwenye maamuzi yako na wengine wanatakiwa kuwapa nafasi wenzao kuwa wanavyotaka kama anavyofanya mungu kwa kuwapa nafasi sawa watu wote.