Wednesday, January 23, 2008

NIMEPOTEZA MDOGO WANGU

Tarehe 17.01/2008 ilikuwa siku mbaya sana kwangu, baada ya kuwa na shaka ya siku tatu kuhusu hali ya mdogo wangu Majaheni T Newa nilipokea habari ya kusikitisha sana kuhusu kifo chake.Mazishi yalifanyika tarehe 19/01/2008.
Majonzi yaliyonikuta hapo sijui kama sio ndugu, jamaa na marafiki kunituliza yangenipeleka mahali ambapo hakuna ambaye angeamini.

Nashukuru wale walioshirikiana nami katika kipindi hicho kigumu na vilevile kuomba msamaha kwa wale ambao tukio hilo liliwagusa na tukashindwa kupatiana habari.