Tuesday, May 16, 2006

Miaka 25 ya kifo cha Bob Marley...

Wiki iliyopita kulikuwa na sherehe na matamasha ya kumkumbuka gwiji la reggae Bob Marley, kama anavyojulikana na wengi,
mwingine alifanya kumbukumbu hiyo kwa njia nyingine, Huyu sio mwingine bali ni rafiki wa karibu sana wa Bob Marley na mpiga gitaa wake maarufu Aston Barret au "Family man". Kumbukumbu yake ilikuwa ni kukumbuka jinsi alivyosaidiana na Bob na wengine wanavyofaidika siku hizi na yeye na ndungu wa marehemu mdogo wake walivyoachwa masikini bila kukumbukwa, madai yaliyomfanya afungue kesi mahakamani na nakala ya hukumu yake
hii hapa .

No comments: